Monday, January 16, 2017

UKATILI WA KIJINSIA


 

Na Dominica Cassian Haule

Ukatili wa kijinsia ni msemo mpana sana. Unagusa binadamu wote wanawake na wanaume. Lakini ni ukweli usiopingika kwamba ukatili wa kijinsia unawaathiri kwa asilimia kubwa wanawake na wasichana kuliko ilivyo kwa wanaume na wavulana. Kuna tafiti lukuki zinazothibitisha.

Wakati wa mababu na mabibi zetu, tulisikia mwanamke kapigwa, kavunjwa mkono, kauawa na kadhalika na kadhalika. Tuliongozwa na tamaduni na kuona maisha ndivyo yanavyotakiwa kuwa.
Raia yenye furaha ni hazina kwa taifa

URITHI

Binafsi, nashawishika kuamini kuwa, ukatili wa kijinsia, umekuwepo tokea mwanzo wa uzao wa binadamu. Ukipitia maandiko mbali mbali, utakuta maandiko, mtu na mkewe. Kwa hili mimi na wewe hatuna budi kujiuliza,  hivi mtu ni nani?. 

 Lakini pia katika maandiko hay ohayo, utakutana na semi binadamu wote. Basi, na tubadilike, tukijua kuwa kwa kuwa neno binadamu wote inamaanisha watu, kwa hiyo, watu hao ni wanawake na wanaume.

Katika familia zetu, kilio kikubwa bado kinaumiza mabinti pale ambapo wazazi/walezi wanapogawa majukumu fulani kuwa ya wasichana na mengine kuwa ya wavulana. Mara nyingi inasahaulika kuwa, vyovyote iwavyo, majukumu ya wasichana yanaweza kuchukua asilimia kubwa ikilinganishwa na asilimia ya majukumu ya wavulana.

Japo kwa asilimia fulani, wakazi wa mijini wameweza kutambua umuhimu wa kuwapa watoto wao majukumu yanayofanana ili mradi hayavuki mipaka. Hii ni njia mojawapo ya kutoa malezi endelevu kwa watoto wote wa kike na wa kiume.

Kadhalika tumeshuhudia, wazazi wanaojadili kutegemea uzao wa watoto wa kiume tu. Na haya yanapatiwa baraka na wanawake pia. Fikiria mama mjamzito  anapolazimika kuomba ajaliwe mtoto wa kiume.Lakini sio kwa matashi yake, bali kwa matashi ya jamii inayomzunguka. Imemtengenezea mtizamo wa kuthamini mtoto wa kiume japoku yeye ni mwanamke.

 HABARI SAHIHI

Vyombo vya habari kwa ujumla wake navyo vinachangia kwa kasi kuwanyima uelewa mpana wananchi ili waachane na vitendo vinavyochangia ukatili wa kijinsia. Haviandiki au kutangaza kwa undani yale yanayopinga ukatili wa kijinsia, ili wananchi wapate upembuzi yakinifu.

Kwa mujibu wa jarida, Jinsia na Vyombo vya Habari Tanzania, lililobeba stadi juu ya mwendelezo wa jinsia na vyombo vya habari  (2010), sauti za wanawake zinasikika pale tu habari inapohusu ukatili wa kijinsia na usawa wa kijinsia. Ambazo zinachukua asilimia 71 na 67. Na habari hizo ni zile za udhalilishaji, mfano ukahaba, mauaji ambayo yametendwa na mwanamke na kadhalika.

 Ingefurahisha na kupongezwa iwapo habari hizo zingekuwa zile zinazoleta maendeleo kwa nchi, ukizingatia kwamba asilimia 70 – 75 ya kazi za uzalishaji hasa sehemu za vijijini hufanywa na wanawake.

La kusikitisha, habari zinazohusu madini kwa mujibu wa jarida hilo hazikupata nafasi katika vyombo vyetu vya habari. Sambamba na hizo, zile zinazohusu  ajira zilipata fursa kwa asilimia kumi tu na zile zinazohusu makazi  zilipatiwa nafasi kwa asilimia kumi kadhalika.

Stadi juu ya mwendelezo wa jinsia na vyombo vya habari Tanzania iliyoratibiwa na asasi isiyo ya kiserikali ya Jinsia na Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika tawi la Tanzania – GEMSAT kwa ufadhili wa asasi isiyo ya kiserikali yenye makao makuu nchini Afrika kusini –‘ Gender Links’, imebaini pia kwamba asilimia sita (6) ya wanawake hubeba utambuzi wa mama, mke au binti kwa upande wa chanzo cha habari. Wakati asilimia nne tu (4) ya wanaume hubeba utambuzi wa baba, mtoto wa kiume au mume.

Hili lina maana gani kwetu. Ni kwamba, mwanamke au msichana  bado anatambuliwa kupitia kwa baba yake mazazi/mlezi au kupitia kwa mumewe.

Japokuwa ukatili wa kijinsia umebainika kufanyika kwa kiwango cha kutisha si tu nchini Tanzania, bali hata katika nchini zilizopo kusimwa mwa Afrika, ni asilimia tatu tu (3) ya habari zinazoandikwa na kutangwa zinaongelea ukatili wa kijinsia.

HISTORIA

Kwa mujibu wa kitabu WANAWAKE WA TANU (Jinsia na Utamaduni katika Kujenga Uzalendo Tanganyika: 1955 – 1965),”wanawake wazalendo walikuwa ni viongozi mashuhuri katika medani zote kwenye ngazi mbalimbali. Wanachama wengi wa TANU walikuwa wanawake na walihusika na majukumu ya kuchangisha fedha, uhamasishaji wa nyumba hadi nyumba na ushawishi wa wanachama katika makundi mbalimbali.”

Kitabu hiki ambacho mwandishi wake ni Susan Geiger, kimetafsiriwa na kurahisishwa na Elieshi lema kwa niaba ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TNGP), kwa lengo mahsusi kuwakumbusha Watanzania na wale wote wanaojali na kuheshimu utu, kutambua kuwa nafasi ya wanawake katika jamii haipaswi kudharauliwa, kubezwa na hata kukejeliwa kwa visingizio mbalimbali. Hili linapotendeka, huu ndio haswa, unyanyasaji kijinsia.

Kitabu hiki kilichosheheni visa mkasa lukuki kinaeleza kwa kina wanawake hawa wazalendo walivyojenga uelewa wa ni nini maana ya utaifa kunzia TANU.

Kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya chama cha Waandishi  wa Habari Wanawake Tanzania ( TAMWA  juu ya ujanyanyasaji wa kijinsia, hali bado ni mbaya. Hali hii ina maana gani kwa serikali, wanaharakati, wanahabari kadhalika Watanzania kwa jumla.

Hii inataka jitihada za ziada katika ngazi zote kuanzia serikali za mitaa hadi serikali kuu.    

 Mwaka 2011, nilisafiri kwa basi  toka kituo kikuu cha mabasi ya abiria yaendayo mikoani cha Ubungo jijini Dar es Salaam, kuelekea wilayani Sengerema mkoani Mwanza.

Kama kawaida ya safari za mikoani, basi hilo likiwa limeenea abiria katika viti vyote, liliondoka katika kituo hicho saa 12.30 asubuhi.

Baada ya mwendo mathalani wa saa mbili, nakumbuka mama mwenye mtoto wa kike mwenye umri kama miaka mitano, alimfuata kondakta na kumweleza kuwa mtoto alihitaji kujisaidia.Kwa mujibu wa mama huyo  alijibiwa asubiri kidogo.

Nakumbuka vizuri kwamba basi lilipamba moto hadi tukafika sehemu ya kuongeza mafuta. Mama yule ambaye alilazimika kurudi katika kiti chake baada ya kuambiwa asubiri, alimjongelea tena dereva kumkumbusha nia yake ya kumpeleka mtoto ajisaidie.

Huwezi kuamini kwamba dereva alimkatalia yule mama na kuendelea kuchanja mbuga. Kilichofuatia ni ukulele mzito toka kwa kina mama waliokuwa ndani ya lile basi. Amini usiamini, dereva alilazimika kusimamisha basi na mama yule kumpeleka mwanaye nje ili ajisaidie.

Ukatili kama huu uleta kilema cha maisha.
Hii kama haitoshi, kina mama ndani ya basi lile kwa umoja wao, walimlaani dereva kadiri kila mmojawao alivyojaliwa na muumba wake. La kushangaza, kina baba walifumba midomo yao kana kwamba hawakusikia wala kuona kilichokuwa kikiendelea baina ya dereva ambaye ni mwanaume mwenzao na mama wa mtoto.

Niliwaza sana na kuwazua kuhusu hili, nikaogopa sana kuhusu maisha yetu iwapo katika kipindi hiki miaka zaidi ya hamsini tokea tujitawale bado tu kina baba hawana uchungu wa kuona kwamba mama awaye yeyote  ni sawa sawa na mama yako. Kadhalika,umwone mtoto wa mwenzio, jirani, rafiki kuwa ni mwanao.

Kutoka Sengerema, kurudi Dar es Salaam nikiwa katika basi tofauti na lile la awali, nilishuhudia kituko kingine kutoka kwa dereva wa basi hilo.

Baada ya mwendo wa karibu kutwa nzima. Majira kama ya saa nane au tisa mchana, aliruhusu abiria kuchimba dawa (kujisaidia) wakati yeye akiongeza mafuta katika basi. Lakini sehemu hiyo ilikuwa na choo chenye vyumba viwili tu. Kimoja kwa wanaume na kimoja kwa wanawake. Hilo kama halitoshi, ni sehemu ambayo mabasi mengi husimama kuongeza mafuta na abiria kuchimba dawa (kujisaidia).

Nakumbuka wakati huo kulikuwa na mabasi takribani matatu. Fikiria abiria wangapi walihitaji huduma hiyo kwa wakati mmoja. Kilichotokea ni kwamba, wanaume kwa jinsi Mungu alivyowajalia, waliweza kujificha ficha na hivyo kuwahi kwenye mabasi kabla ya wanawake.

Hali hiyo ilisababisha wanawake washindwe kujikamilisha kabla ya muda ambao ulitolewa. Dereva   wa basi nililopanda akaondoa basi bila ya kujali kuwa, kuna wanawake walikuwahawajaingia licha ya kuelezwa. Kama kawaida akapigiwa kelele na wasamaria wema na kutishiwa kuwa wangempiga laiti angewaacha kina mama hao.

Visa mkasa hivi viwili, ni vionjo tu nilivyokupa ndugu MTANZANIA. Katika kisa mkasa cha mwanzo, unaona wazi ni jinsi gani ukatili wa kijinsia unavyotesa wanawake. Mama huyu na mwanae wa kike wote wameangukia katika lindi la kufanyiwa ukatili.

MTANZANIA mwenzangu ni mara ngapi tumeshuhudia tukiwa safarini, wanaume wanavyowaomba madereva wasimame ili wajisaidie. Tena, kila wanapojisikia, wala hawajali kama ni mahali pa wazi au penye usiri.Tena wako baadhi ya madereva, wanaotumia fursa za wanaume kuwasimamisha  mara kwa mara, kuwapa pia  fursa hiyo abiria wengine, bila kujali kuwa sehemu husika haitawafaa wanawake. Huu ni UKATILI WA KIJINSIA.

Kisa mkasa cha pili, kadhalika. Ni wajibu wa madereva kuhakikisha kuwa sehemu wanazowapeleka abiria wao ‘kuchimba dawa’ zinakidhi mahitaji ya wanawake na wanaume kwa wakati mmoja?. Iwapo hazikidhi, basi watafute maeneo ambayo hayatakuwa ya  karaha hususan kwa wanawake na wasichana.

Jambo lingine kubwa na la msingi ni kwamba, mara nyingi wasafiri hawa huandamana na watu wanaowaheshimu. Ambao kwa mujibu wa tamaduni zetu, hawawezi wakaandamana nao ‘kuchimba dawa’ katika eneo moja. Lazima mmoja awe mbali na mwingine. Mfano, mama amesafiri na babake mzazi/baba mkwe. Au mtoto mwenye umri mkubwa amesafiri na mama yake mzazi/mama mkwe. Katika haya, WATANZANIA wenzangu tusidanganyane kwamba tunakwenda na wakati. Haya hayana wakati, tumezaliwa tumeyakuta na tutaendelea kuyaenzi kwa faida ya vizazi vijavyo.

 

Dominica Cassian Haule, ni Mwandishi wa Habari / Mchambuzi wa Masuala ya Jinsia   na Mwenyekiti wa Asasi ya Jinsia na Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania – GEMSAT.

dominicahaule@yahoo.com

 

 

 

   

UKATILI WA KIJINSIA

Na Dominica Cassian Haule

Ukatili wa kijinsia ni msemo mpana sana. Unagusa binadamu wote wanawake na wanaume. Lakini ni ukweli usiopingika kwamba ukatili wa kijinsia unawaathiri kwa asilimia kubwa wanawake na wasichana kuliko ilivyo kwa wanaume na wavulana. Kuna tafiti lukuki zinazothibitisha. Wakati wa mababu na mabibi zetu, tulisikia mwanamke kapigwa, kavunjwa mkono, kauawa na kadhalika na kadhalika. Tuliongozwa na tamaduni na kuona maisha ndivyo yanavyotakiwa kuwa.

URITHI Binafsi, nashawishika kuamini kuwa, ukatili wa kijinsia, umekuwepo tokea mwanzo wa uzao wa binadamu. Ukipitia maandiko mbali mbali, utakuta maandiko, mtu na mkewe. Kwa hili mimi na wewe hatuna budi kujiuliza, hivi mtu ni nani?  Lakini pia katika maandiko hay ohayo, utakutana na semi binadamu wote. Basi, na tubadilike, tukijua kuwa kwa kuwa neno binadamu wote inamaanisha watu, kwa hiyo, watu hao ni wanawake na wanaume.

Katika familia zetu, kilio kikubwa bado kinaumiza mabinti pale ambapo wazazi/walezi wanapogawa majukumu fulani kuwa ya wasichana na mengine kuwa ya wavulana. Mara nyingi inasahaulika kuwa, vyovyote iwavyo, majukumu ya wasichana yanaweza kuchukua asilimia kubwa ikilinganishwa na asilimia ya majukumu ya wavulana.

Japo kwa asilimia fulani, wakazi wa mijini wameweza kutambua umuhimu wa kuwapa watoto wao majukumu yanayofanana ili mradi hayavuki mipaka. Hii ni njia mojawapo ya kutoa malezi endelevu kwa watoto wote wa kike na wa kiume. Kadhalika tumeshuhudia, wazazi wanaojadili kutegemea uzao wa watoto wa kiume tu. Na haya yanapatiwa baraka na wanawake pia. Fikiria mama mjamzito anapolazimika kuomba ajaliwe mtoto wa kiume.

Lakini sio kwa matashi yake, bali kwa matashi ya jamii inayomzunguka. Imemtengenezea mtizamo wa kuthamini mtoto wa kiume japoku yeye ni mwanamke. HABARI SAHIHI Vyombo vya habari kwa ujumla wake navyo vinachangia kwa kasi kuwanyima uelewa mpana wananchi ili waachane na vitendo vinavyochangia ukatili wa kijinsia. Haviandiki au kutangaza kwa undani yale yanayopinga ukatili wa kijinsia, ili wananchi wapate upembuzi yakinifu. Kwa mujibu wa jarida, Jinsia na Vyombo vya Habari Tanzania, lililobeba stadi juu ya mwendelezo wa jinsia na vyombo vya habari (2010), sauti za wanawake zinasikika pale tu habari inapohusu ukatili wa kijinsia na usawa wa kijinsia. Ambazo zinachukua asilimia 71 na 67.

Na habari hizo ni zile za udhalilishaji, mfano ukahaba, mauaji ambayo yametendwa na mwanamke na kadhalika. Ingefurahisha na kupongezwa iwapo habari hizo zingekuwa zile zinazoleta maendeleo kwa nchi, ukizingatia kwamba asilimia 70 – 75 ya kazi za uzalishaji hasa sehemu za vijijini hufanywa na wanawake. La kusikitisha, habari zinazohusu madini kwa mujibu wa jarida hilo hazikupata nafasi katika vyombo vyetu vya habari. Sambamba na hizo, zile zinazohusu ajira zilipata fursa kwa asilimia kumi tu na zile zinazohusu makazi zilipatiwa nafasi kwa asilimia kumi kadhalika.

Stadi juu ya mwendelezo wa jinsia na vyombo vya habari Tanzania iliyoratibiwa na asasi isiyo ya kiserikali ya Jinsia na Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika tawi la Tanzania – GEMSAT kwa ufadhili wa asasi isiyo ya kiserikali yenye makao makuu nchini Afrika kusini –‘ Gender Links’, imebaini pia kwamba asilimia sita (6) ya wanawake hubeba utambuzi wa mama, mke au binti kwa upande wa chanzo cha habari. Wakati asilimia nne tu (4) ya wanaume hubeba utambuzi wa baba, mtoto wa kiume au mume. Hili lina maana gani kwetu. Ni kwamba, mwanamke au msichana bado anatambuliwa kupitia kwa baba yake mazazi/mlezi au kupitia kwa mumewe.

Tanzania yenye raia wa kike na kiume
wenye furaha inawezekana
Japokuwa ukatili wa kijinsia umebainika kufanyika kwa kiwango cha kutisha si tu nchini Tanzania, bali hata katika nchini zilizopo kusimwa mwa Afrika, ni asilimia tatu tu (3) ya habari zinazoandikwa na kutangwa zinaongelea ukatili wa kijinsia. HISTORIA Kwa mujibu wa kitabu WANAWAKE WA TANU (Jinsia na Utamaduni katika Kujenga Uzalendo Tanganyika: 1955 – 1965),”wanawake wazalendo walikuwa ni viongozi mashuhuri katika medani zote kwenye ngazi mbalimbali.

Wanachama wengi wa TANU walikuwa wanawake na walihusika na majukumu ya kuchangisha fedha, uhamasishaji wa nyumba hadi nyumba na ushawishi wa wanachama katika makundi mbalimbali.” Kitabu hiki ambacho mwandishi wake ni Susan Geiger, kimetafsiriwa na kurahisishwa na Elieshi lema kwa niaba ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TNGP), kwa lengo mahsusi kuwakumbusha Watanzania na wale wote wanaojali na kuheshimu utu, kutambua kuwa nafasi ya wanawake katika jamii haipaswi kudharauliwa, kubezwa na hata kukejeliwa kwa visingizio mbalimbali. Hili linapotendeka, huu ndio haswa, unyanyasaji kijinsia. Kitabu hiki kilichosheheni visa mkasa lukuki kinaeleza kwa kina wanawake hawa wazalendo walivyojenga uelewa wa ni nini maana ya utaifa kunzia TANU.

Kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania ( TAMWA juu ya ujanyanyasaji wa kijinsia, hali bado ni mbaya. Hali hii ina maana gani kwa serikali, wanaharakati, wanahabari kadhalika Watanzania kwa jumla. Hii inataka jitihada za ziada katika ngazi zote kuanzia serikali za mitaa hadi serikali kuu. Mwaka 2011, nilisafiri kwa basi toka kituo kikuu cha mabasi ya abiria yaendayo mikoani cha Ubungo jijini Dar es Salaam, kuelekea wilayani Sengerema mkoani Mwanza.

Kama kawaida ya safari za mikoani, basi hilo likiwa limeenea abiria katika viti vyote, liliondoka katika kituo hicho saa 12.30 asubuhi. Baada ya mwendo mathalani wa saa mbili, nakumbuka mama mwenye mtoto wa kike mwenye umri kama miaka mitano, alimfuata kondakta na kumweleza kuwa mtoto alihitaji kujisaidia.Kwa mujibu wa mama huyo alijibiwa asubiri kidogo. Nakumbuka vizuri kwamba basi lilipamba moto hadi tukafika sehemu ya kuongeza mafuta. Mama yule ambaye alilazimika kurudi katika kiti chake baada ya kuambiwa asubiri, alimjongelea tena dereva kumkumbusha nia yake ya kumpeleka mtoto ajisaidie. Huwezi kuamini kwamba dereva alimkatalia yule mama na kuendelea kuchanja mbuga.

Kilichofuatia ni ukulele mzito toka kwa kina mama waliokuwa ndani ya lile basi. Amini usiamini, dereva alilazimika kusimamisha basi na mama yule kumpeleka mwanaye nje ili ajisaidie. Hii kama haitoshi, kina mama ndani ya basi lile kwa umoja wao, walimlaani dereva kadiri kila mmojawao alivyojaliwa na muumba wake. La kushangaza, kina baba walifumba midomo yao kana kwamba hawakusikia wala kuona kilichokuwa kikiendelea baina ya dereva ambaye ni mwanaume mwenzao na mama wa mtoto. Niliwaza sana na kuwazua kuhusu hili, nikaogopa sana kuhusu maisha yetu iwapo katika kipindi hiki miaka zaidi ya hamsini tokea tujitawale bado tu kina baba hawana uchungu wa kuona kwamba mama awaye yeyote ni sawa sawa na mama yako. Kadhalika,umwone mtoto wa mwenzio, jirani, rafiki kuwa ni mwanao. Kutoka Sengerema, kurudi Dar es Salaam nikiwa katika basi tofauti na lile la awali, nilishuhudia kituko kingine kutoka kwa dereva wa basi hilo.

Baada ya mwendo wa karibu kutwa nzima. Majira kama ya saa nane au tisa mchana, aliruhusu abiria kuchimba dawa (kujisaidia) wakati yeye akiongeza mafuta katika basi. Lakini sehemu hiyo ilikuwa na choo chenye vyumba viwili tu. Kimoja kwa wanaume na kimoja kwa wanawake. Hilo kama halitoshi, ni sehemu ambayo mabasi mengi husimama kuongeza mafuta na abiria kuchimba dawa (kujisaidia). Nakumbuka wakati huo kulikuwa na mabasi takribani matatu. Fikiria abiria wangapi walihitaji huduma hiyo kwa wakati mmoja. Kilichotokea ni kwamba, wanaume kwa jinsi Mungu alivyowajalia, waliweza kujificha ficha na hivyo kuwahi kwenye mabasi kabla ya wanawake.

Hali hiyo ilisababisha wanawake washindwe kujikamilisha kabla ya muda ambao ulitolewa. Dereva wa basi nililopanda akaondoa basi bila ya kujali kuwa, kuna wanawake walikuwahawajaingia licha ya kuelezwa. Kama kawaida akapigiwa kelele na wasamaria wema na kutishiwa kuwa wangempiga laiti angewaacha kina mama hao. Visa mkasa hivi viwili, ni vionjo tu nilivyokupa ndugu MTANZANIA. Katika kisa mkasa cha mwanzo, unaona wazi ni jinsi gani ukatili wa kijinsia unavyotesa wanawake.

Ukatili wa kupigana kati ya mke na mume
mara nyingi wanawake hudhurika zaidi.
Mama huyu na mwanae wa kike wote wameangukia katika lindi la kufanyiwa ukatili. MTANZANIA mwenzangu ni mara ngapi tumeshuhudia tukiwa safarini, wanaume wanavyowaomba madereva wasimame ili wajisaidie. Tena, kila wanapojisikia, wala hawajali kama ni mahali pa wazi au penye usiri.Tena wako baadhi ya madereva, wanaotumia fursa za wanaume kuwasimamisha mara kwa mara, kuwapa pia fursa hiyo abiria wengine, bila kujali kuwa sehemu husika haitawafaa wanawake. Huu ni UKATILI WA KIJINSIA.

Kisa mkasa cha pili, kadhalika. Ni wajibu wa madereva kuhakikisha kuwa sehemu wanazowapeleka abiria wao ‘kuchimba dawa’ zinakidhi mahitaji ya wanawake na wanaume kwa wakati mmoja?. Iwapo hazikidhi, basi watafute maeneo ambayo hayatakuwa ya karaha hususan kwa wanawake na wasichana. Jambo lingine kubwa na la msingi ni kwamba, mara nyingi wasafiri hawa huandamana na watu wanaowaheshimu. Ambao kwa mujibu wa tamaduni zetu, hawawezi wakaandamana nao ‘kuchimba dawa’ katika eneo moja. Lazima mmoja awe mbali na mwingine.

Mfano, mama amesafiri na babake mzazi/baba mkwe. Au mtoto mwenye umri mkubwa amesafiri na mama yake mzazi/mama mkwe. Katika haya, WATANZANIA wenzangu tusidanganyane kwamba tunakwenda na wakati. Haya hayana wakati, tumezaliwa tumeyakuta na tutaendelea kuyaenzi kwa faida ya vizazi vijavyo. Dominica Cassian Haule, ni Mwandishi wa Habari / Mchambuzi wa Masuala ya Jinsia na Mwenyekiti wa Asasi ya Jinsia na Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania – GEMSAT. dominicahaule@yahoo.com