Wednesday, September 20, 2017

COMMUNITY RADIO GENDER & MEDIA POLICY ASSESSMENT REPORT



BRIEF ACTIVITY REPORT OF THE COMMUNITY MEDIA FEEDBACK WORKSHOP ON THE ASSESSMENT REPORT ON GENDER MAINSTREAMING

Community Radio Representatives at the workshop in Kilosa.


Gerald Malekela presenter and reporter from Nuru FM -Iringa narrated their experiences in gender implementation at the media house during the workshop in Kilosa.


 



 

Submitted by

The Gender and Media in Southern Africa, Tanzania Network – August 2015

 

BRIEF ACTIVITY REPORT OF THE WORKSHOP ON MEDIA ENGAGEMENT STRATEGY

1.                             Background information of the activity

Activity Title:
Brief activity report of the community media feedback workshop on the assessment report on gender mainstreaming
 
Location of Activity:
Kilosa
Activity Dates:
20th – 22nd August 2015

Activity Description:

The three-day workshop was intended to bring together community radio managers/practitioners to be  introduced to UNESCOs Gender Sensitive Indicators , to discuss the report findings of the assessment on the existing gender gaps in the community media especially radios and  draw the way forward on how to bridge the existing gaps.
Target Group:
The targeted groups were community media managers/practitioners from Kilosa FM, Kyela FM, Mtegani FM, Kitulo FM, Fadhila FM, Dodoma FM, Nuru FM, Pambazuko, Daraja newspaper, Mtukwao, Boma Hai Radio and Pangani FM.
Objectives: (as per project proposal)
  • The community media will be able to identify the existing gender equality gaps within the content production and all the other aspects of their operations;
  • Community media stations will improve their gender responsiveness by applying the in place UNESCO Gender Sensitive Indicators; and
  • The communities will benefit from the improved gender –sensitive news and current affairs content.
 
Participating Officers:
Organization
Sex
Designation
F
M
GEMSAT
3
1
Facilitators
 
 
 
 
 
 
 
 


2.  Participants

Organization
Sex
Designation
F
M
Community media managers/practitioners
4
9
from Kilosa FM, Kyela FM, Mtegani FM, Kitulo FM, Fadhila FM, Dodoma FM, Nuru FM, Pambazuko, Daraja newspaper, Mtukwao, Boma Hai Radio and Pangani FM

 

 

3.0 Issues emerged during the workshop


  1. Men still dominate media sources of information since 2003 Gender and Media Baseline Survey when women sources were 16%, 2005 Global Monitoring Project study when the women sources were 18% to 2010 Gender and Media Progress Study when women sources were 21% and Global Media Monitoring Study when the sources were 24%.  So there were slightly changes since 2003.
  2. All the previous studies, however, did not include community media.
  3. Media fail to break the glass ceiling by segregating issues covered according to specific sex. For instance it is not easy to see media is mainstreaming gender in stories related to football matches.
  4. Tanzanian media especially during the elections is divided into three groups – lap dog which serves the interest of master, guard dog which is to serve the vested interest and watch dog which serves the public interest. But there is a reason why they do so. First is working conditions of journalists, existence of harsh media laws, small capital base of media houses and reflection of its own society.
  5. Some community media have established policies requiring the media to concentrate much on local information rather than national and international in order to server better the community.
  6. Existence of gender gap within community media and even the mainstream is sometimes caused by the government system whereby most figures who can make news are men. But women can easily be mainstreamed by approaching the ordinary citizens to get their comments and views.
  7. Voice insert can show the reality and simplify gender monitoring as is easy to know the sex of source. Sometime sources cannot be identified through names as there are names that are unisex.
 

 

4. Results of the activity

  1. Thirteen participants from community media out of 14 invitees attended the workshop. Only one participant from Mtukwao did not attend the workshop.
  2. The participants were able to identify challenges related to accessing women as information sources for their media houses and committed to devise mechanism to get them even if they are not popular such as ordinary citizens for comments and opinions.
  3. Participants were able to listen to the assessment and comments on the results of their own media. They were also able to listen some news bulletin from their media houses and monitor themselves the existing gender gaps. At the end of the day they accepted that the assessment reflected the reality of their media houses.
  4. Participants came up with resolutions submitted to the guest of honour and also committed to submit them to the management of their media houses for further improvements. The resolutions place responsibilities to the management of media houses, GEMSAT and UNESCO and to the participants themselves. The resolutions are attached as annex.
  5. The Guest of Honour, The District Executive Director for Kilosa committed to support the Kilosa community radio as the resolutions were not  new, they included issues that have been in the discussion for long between District Council and the radio management.
 
 




5. Challenges

  • One community radio station, Mtukwao of Mtwara did not send representative to the workshop thus presenting the missed opportunity for the station.
  • Not all participants attended were from the decision making positions. But they committed themselves to send the workshop resolutions to the decision making people.

 

6. Lessons learned

  • Capacity building of community media based on facts and figures and evidence of the existing gender gaps has a big chance to promote gender equality in the news and current affairs of community media in Tanzania.

 

7. Reporting person

Name:
Gladness H. Munuo
Title:
Coordinator
 
 
 

 

 

Annex No. 1 Participants list for Community Media Workshop in Kilosa from 20th August to 23rd August, 20015

No.
NAME
SEX
ORGANISATION/MEDIA HOUSE
POSITION
PHONE
E-MAIL
1
Zilpa joseph gappy
F
Triple a fm
Sub – Editor
0764713084
2
Gasper Jospeh
M
Boma Hai FM
Presenter
0766-536061
3
Aloycia Mhina
F
Kilosa FM
Presenter
0787 091531
4
Masoud Maulidi
M
Kyela FM
Presenter
0768 767179
5
Edwin Mpokasye
M
Radio Fadhila
Director
0756 923376
6
Ergon Elly
M
Kitulo FM
Presenter
0768 511 373
7
Lucas Godwin
M
Dodoma FM
Assistant  Manager
0716057615
8
Gerald E. Malekela
M
Nuru FM
Presenter
0715 779233
9
Winifrida Mayao
F
Zenj FM
Radio Manager
0655 780 790
10
Martha james
F
Pangani FM
Presenter
0656899270
11
Shaaban Ali
M
Mtengani FM
Assistant Manager
0777 888084
12
Isidory mtunda
M
Pambazuko FM
Presenter
0782780325
13
Richard Shagungu
M
Kilosa FM
Manager
0787 411344
14
Cecilia Stephen
F
GEMSAT
Treasurer
0717864677
15
Gladness Hemed Munuo
F
GEMSAT
Coordinator
 
 
16
Dominica Haule
F
GEMSAT
CHAIRPERSON
 
 
17
Marko Gideon
M
GEMSAT
Secretary
0717422829
 

                       

 

Annex No. 2 Resolutions

 

TAARIFA YA WARSHA WA UANDAAJI WA VIPINDI NA HABARI ZA JINSIA KWA REDIO JAMII  TAREHE 20 – 22, AGOSTI 2015

 

 

UTANGULIZI:

Warsha ya uandaaji wa vipindi na habari za kijinsia iliyoandaliwa na taasisi  isiyo ya kiserikali  inayoshughulika na maswala ya kijinsia ,kusini mwa jangwa la sahara Tanzania GEMSAT yenye lengo la kupata mrejesho wa makubaliano yaliyofanyika wakati wa kuaanda sera ya jisia na habari ambayo yaliwashirikisha  vyombo vya habari vya kijamii.

Redio ambazo zimeshiriki katika warsha hii ni Kilosa FM, Pambazuko Fm ifakara, Zenj FM Zanzibar, Nuru FM Iringa, Pangani FM , Kitulo FM Makete, Boma Hai Kilimanjaro,Triple A Arusha,Mtegani FM Zanzibar, Kyela FM , Dodoma FM, Fadhila FM Masasi.

 

. Vyombo vya habari vyenyewe vimeonekana kutekeleza sera ya jinsia na habari  kwenye ajira na ufanyaji wa vipindi.

 

2. Kwakiasi flani vyombo vya habari vinaripoti maswala ya jinsia.

 

3. Baadhi ya redio zina   vipindi vya moja kwa moja vinavyohusu jinsia . mfano : wanwake kwanza –pambazuko fm na harakati za wanawake  zenj fm.

 

Vipindi  vimeonyesha matokeo chanya kwa baadhi ya maeneo : kwa mifano halisi kupitia kipindi cha ulimwengu wa wanawake Nuru FM wanawake wameweza kujitokeza kuwania nafasi za uongozi ngazi ya udiwani na ubunge tofauti na miaka ya nyuma, na kipindi cha ndoa na familia Boma Hai FM na kipindi cha Sauti ya mwanamke Pangani FM wanawake wamekuwa wazi kueleza matatizo yao katika vyombo vya habari tofauti na hapo awali.

 

5. Wanawake wamekuwa na mwamko wa kushiriki katika vipindi na kuchangia mijadala mbalimbali katika vipindi.

 

CHANGAMOTO:

1. Bado uwiano wa jinsia  kwa kiasi flani hauridhishi.

Changamoto ya kifedha ambapo inapelekea :

      Vipindi kutofanyika ipasavyo

      Wafanyakazi kuondoka kutoka na malipo madogo.

      Urasimu katika utoaji wa fedha  kwaajili ya utekelezaji wa majuku punde inapohitajika, ikiwemo uandaaji wavipindi na habari .

2. Baadhi ya wadau na viongozi kupuuza vyombo vya habari vya kijamii.

3. Changamoto ya elimu kwa wanahabari juu ya uaandaji wa vipindi vya jinsia.

4. Wamiliki Kuingilia majukumu ya kitaaluma. Mfano mmiliki anaweza kutoa agizo la kutangazwa au kutotangazwa taarifa au kurusha kipindi kwa maslahi yake kinyume na sera ya utangazaji na mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA.

 

MAAZIMIO

1. Vyombo vya  habari vinatakiwa kuzingitia uwiano wa jinsia kulingana na sera ya jinsia na habari katika uajiri na uratibu wa vipindi.

2. Vyombo vya habari viachwe viwe huru ili viweze kujiendesha.

Wamiliki wa vyombo vya habari waone umuhimu na kuweka utaratibu wa kuwaendeleza wafanyakazi wao Kielimu.

3. Chombo cha habari kitengeneze mazingira mazuri ya uhusiano na wadau wao.

Wamiliki waache vyombo viwe huru katika kutekeleza majukumu yake.

4. Vyombo vya habari viongeze vipindi na habari za zinazolenga   usawa wa jinsia kwa kuzingati sera ya jinsia na habari.

 

 

GEMSAT na wadau wengine wandelee kutoa mafunzo ya mara kwa ya maswala ya jinsia ikiwezekana semina zefanyike katika maeneo ambayo tatizo hili ni kubwa.

6. Urasimu uondoke katika utoaji wa fedha za kuandalia vipi na utekelezaji wa majukumu yote ya chombo.

Redio ziwe na account zao  ili kuwe na urahisi wa upatikanaji wa fedha.

7. Vituo viweke utaratibu mzuri wa malipo kwa kwa wafanyakazi wake ili wasiondoke na kuzorotesha vipindi.

Vituo viboreshe njia za kuongeza mapato kwa kutafuta wafadhili ,matangazo .

8. Washiriki wapeleke mrejesho wa mafunzo haya  kwa wenzao katika vituo vyao vya redio  ili kuunganisha nguvu katika kutekeleza sera ya jinsia na habari. 

 

Redio ziwe na account zao  ili kuwe na urahisi wa upatikanaji wa fedha.

10. Vituo viweke utaratibu mzuri wa malipo kwa kwa wafanyakazi wake ili wasiondoke na kuzorotesha vipindi.

11. Vituo viboreshe njia za kuongeza mapato kwa kutafuta wafadhili ,matangazo .

12. Washiriki wapeleke mrejesho wa mafunzo haya  kwa wenzao katika vituo vyao vya redio  ili kuunganisha nguvu katika kutekeleza sera ya jinsia na habari. 

 

USHAURI

1. Iandaliwe  semina ya tathmini ya maazimio haya ,ikiwezekana kabla ya mwaka huu kuisha TUKIAMINI KUWA TUNATAKA KUKIMBIA SIO KUTEMBEA.

 

2. GEMSAT waratibu na kufuatilia vipindi mbalimbali vya habari na jinsia vinavyoandaliwa na redio za kijamii kwa kutengeneza mfumo utakao waunganisha wote. Mfano kipindi cha redio moja kurusha redio nyingine na kutoa motisha kwa muandaaji.    

 

HITIMISHO

Iwapo vituo vya redio jamii vitafanikiwa kutekeleza maazimio haya utekelezaji wa sera ya jinsia na habari kwa kiasi kikubwa itafikiwa na kupunguza tatizo hili katika jamii.

 


Monday, January 16, 2017

UKATILI WA KIJINSIA


 

Na Dominica Cassian Haule

Ukatili wa kijinsia ni msemo mpana sana. Unagusa binadamu wote wanawake na wanaume. Lakini ni ukweli usiopingika kwamba ukatili wa kijinsia unawaathiri kwa asilimia kubwa wanawake na wasichana kuliko ilivyo kwa wanaume na wavulana. Kuna tafiti lukuki zinazothibitisha.

Wakati wa mababu na mabibi zetu, tulisikia mwanamke kapigwa, kavunjwa mkono, kauawa na kadhalika na kadhalika. Tuliongozwa na tamaduni na kuona maisha ndivyo yanavyotakiwa kuwa.
Raia yenye furaha ni hazina kwa taifa

URITHI

Binafsi, nashawishika kuamini kuwa, ukatili wa kijinsia, umekuwepo tokea mwanzo wa uzao wa binadamu. Ukipitia maandiko mbali mbali, utakuta maandiko, mtu na mkewe. Kwa hili mimi na wewe hatuna budi kujiuliza,  hivi mtu ni nani?. 

 Lakini pia katika maandiko hay ohayo, utakutana na semi binadamu wote. Basi, na tubadilike, tukijua kuwa kwa kuwa neno binadamu wote inamaanisha watu, kwa hiyo, watu hao ni wanawake na wanaume.

Katika familia zetu, kilio kikubwa bado kinaumiza mabinti pale ambapo wazazi/walezi wanapogawa majukumu fulani kuwa ya wasichana na mengine kuwa ya wavulana. Mara nyingi inasahaulika kuwa, vyovyote iwavyo, majukumu ya wasichana yanaweza kuchukua asilimia kubwa ikilinganishwa na asilimia ya majukumu ya wavulana.

Japo kwa asilimia fulani, wakazi wa mijini wameweza kutambua umuhimu wa kuwapa watoto wao majukumu yanayofanana ili mradi hayavuki mipaka. Hii ni njia mojawapo ya kutoa malezi endelevu kwa watoto wote wa kike na wa kiume.

Kadhalika tumeshuhudia, wazazi wanaojadili kutegemea uzao wa watoto wa kiume tu. Na haya yanapatiwa baraka na wanawake pia. Fikiria mama mjamzito  anapolazimika kuomba ajaliwe mtoto wa kiume.Lakini sio kwa matashi yake, bali kwa matashi ya jamii inayomzunguka. Imemtengenezea mtizamo wa kuthamini mtoto wa kiume japoku yeye ni mwanamke.

 HABARI SAHIHI

Vyombo vya habari kwa ujumla wake navyo vinachangia kwa kasi kuwanyima uelewa mpana wananchi ili waachane na vitendo vinavyochangia ukatili wa kijinsia. Haviandiki au kutangaza kwa undani yale yanayopinga ukatili wa kijinsia, ili wananchi wapate upembuzi yakinifu.

Kwa mujibu wa jarida, Jinsia na Vyombo vya Habari Tanzania, lililobeba stadi juu ya mwendelezo wa jinsia na vyombo vya habari  (2010), sauti za wanawake zinasikika pale tu habari inapohusu ukatili wa kijinsia na usawa wa kijinsia. Ambazo zinachukua asilimia 71 na 67. Na habari hizo ni zile za udhalilishaji, mfano ukahaba, mauaji ambayo yametendwa na mwanamke na kadhalika.

 Ingefurahisha na kupongezwa iwapo habari hizo zingekuwa zile zinazoleta maendeleo kwa nchi, ukizingatia kwamba asilimia 70 – 75 ya kazi za uzalishaji hasa sehemu za vijijini hufanywa na wanawake.

La kusikitisha, habari zinazohusu madini kwa mujibu wa jarida hilo hazikupata nafasi katika vyombo vyetu vya habari. Sambamba na hizo, zile zinazohusu  ajira zilipata fursa kwa asilimia kumi tu na zile zinazohusu makazi  zilipatiwa nafasi kwa asilimia kumi kadhalika.

Stadi juu ya mwendelezo wa jinsia na vyombo vya habari Tanzania iliyoratibiwa na asasi isiyo ya kiserikali ya Jinsia na Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika tawi la Tanzania – GEMSAT kwa ufadhili wa asasi isiyo ya kiserikali yenye makao makuu nchini Afrika kusini –‘ Gender Links’, imebaini pia kwamba asilimia sita (6) ya wanawake hubeba utambuzi wa mama, mke au binti kwa upande wa chanzo cha habari. Wakati asilimia nne tu (4) ya wanaume hubeba utambuzi wa baba, mtoto wa kiume au mume.

Hili lina maana gani kwetu. Ni kwamba, mwanamke au msichana  bado anatambuliwa kupitia kwa baba yake mazazi/mlezi au kupitia kwa mumewe.

Japokuwa ukatili wa kijinsia umebainika kufanyika kwa kiwango cha kutisha si tu nchini Tanzania, bali hata katika nchini zilizopo kusimwa mwa Afrika, ni asilimia tatu tu (3) ya habari zinazoandikwa na kutangwa zinaongelea ukatili wa kijinsia.

HISTORIA

Kwa mujibu wa kitabu WANAWAKE WA TANU (Jinsia na Utamaduni katika Kujenga Uzalendo Tanganyika: 1955 – 1965),”wanawake wazalendo walikuwa ni viongozi mashuhuri katika medani zote kwenye ngazi mbalimbali. Wanachama wengi wa TANU walikuwa wanawake na walihusika na majukumu ya kuchangisha fedha, uhamasishaji wa nyumba hadi nyumba na ushawishi wa wanachama katika makundi mbalimbali.”

Kitabu hiki ambacho mwandishi wake ni Susan Geiger, kimetafsiriwa na kurahisishwa na Elieshi lema kwa niaba ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TNGP), kwa lengo mahsusi kuwakumbusha Watanzania na wale wote wanaojali na kuheshimu utu, kutambua kuwa nafasi ya wanawake katika jamii haipaswi kudharauliwa, kubezwa na hata kukejeliwa kwa visingizio mbalimbali. Hili linapotendeka, huu ndio haswa, unyanyasaji kijinsia.

Kitabu hiki kilichosheheni visa mkasa lukuki kinaeleza kwa kina wanawake hawa wazalendo walivyojenga uelewa wa ni nini maana ya utaifa kunzia TANU.

Kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya chama cha Waandishi  wa Habari Wanawake Tanzania ( TAMWA  juu ya ujanyanyasaji wa kijinsia, hali bado ni mbaya. Hali hii ina maana gani kwa serikali, wanaharakati, wanahabari kadhalika Watanzania kwa jumla.

Hii inataka jitihada za ziada katika ngazi zote kuanzia serikali za mitaa hadi serikali kuu.    

 Mwaka 2011, nilisafiri kwa basi  toka kituo kikuu cha mabasi ya abiria yaendayo mikoani cha Ubungo jijini Dar es Salaam, kuelekea wilayani Sengerema mkoani Mwanza.

Kama kawaida ya safari za mikoani, basi hilo likiwa limeenea abiria katika viti vyote, liliondoka katika kituo hicho saa 12.30 asubuhi.

Baada ya mwendo mathalani wa saa mbili, nakumbuka mama mwenye mtoto wa kike mwenye umri kama miaka mitano, alimfuata kondakta na kumweleza kuwa mtoto alihitaji kujisaidia.Kwa mujibu wa mama huyo  alijibiwa asubiri kidogo.

Nakumbuka vizuri kwamba basi lilipamba moto hadi tukafika sehemu ya kuongeza mafuta. Mama yule ambaye alilazimika kurudi katika kiti chake baada ya kuambiwa asubiri, alimjongelea tena dereva kumkumbusha nia yake ya kumpeleka mtoto ajisaidie.

Huwezi kuamini kwamba dereva alimkatalia yule mama na kuendelea kuchanja mbuga. Kilichofuatia ni ukulele mzito toka kwa kina mama waliokuwa ndani ya lile basi. Amini usiamini, dereva alilazimika kusimamisha basi na mama yule kumpeleka mwanaye nje ili ajisaidie.

Ukatili kama huu uleta kilema cha maisha.
Hii kama haitoshi, kina mama ndani ya basi lile kwa umoja wao, walimlaani dereva kadiri kila mmojawao alivyojaliwa na muumba wake. La kushangaza, kina baba walifumba midomo yao kana kwamba hawakusikia wala kuona kilichokuwa kikiendelea baina ya dereva ambaye ni mwanaume mwenzao na mama wa mtoto.

Niliwaza sana na kuwazua kuhusu hili, nikaogopa sana kuhusu maisha yetu iwapo katika kipindi hiki miaka zaidi ya hamsini tokea tujitawale bado tu kina baba hawana uchungu wa kuona kwamba mama awaye yeyote  ni sawa sawa na mama yako. Kadhalika,umwone mtoto wa mwenzio, jirani, rafiki kuwa ni mwanao.

Kutoka Sengerema, kurudi Dar es Salaam nikiwa katika basi tofauti na lile la awali, nilishuhudia kituko kingine kutoka kwa dereva wa basi hilo.

Baada ya mwendo wa karibu kutwa nzima. Majira kama ya saa nane au tisa mchana, aliruhusu abiria kuchimba dawa (kujisaidia) wakati yeye akiongeza mafuta katika basi. Lakini sehemu hiyo ilikuwa na choo chenye vyumba viwili tu. Kimoja kwa wanaume na kimoja kwa wanawake. Hilo kama halitoshi, ni sehemu ambayo mabasi mengi husimama kuongeza mafuta na abiria kuchimba dawa (kujisaidia).

Nakumbuka wakati huo kulikuwa na mabasi takribani matatu. Fikiria abiria wangapi walihitaji huduma hiyo kwa wakati mmoja. Kilichotokea ni kwamba, wanaume kwa jinsi Mungu alivyowajalia, waliweza kujificha ficha na hivyo kuwahi kwenye mabasi kabla ya wanawake.

Hali hiyo ilisababisha wanawake washindwe kujikamilisha kabla ya muda ambao ulitolewa. Dereva   wa basi nililopanda akaondoa basi bila ya kujali kuwa, kuna wanawake walikuwahawajaingia licha ya kuelezwa. Kama kawaida akapigiwa kelele na wasamaria wema na kutishiwa kuwa wangempiga laiti angewaacha kina mama hao.

Visa mkasa hivi viwili, ni vionjo tu nilivyokupa ndugu MTANZANIA. Katika kisa mkasa cha mwanzo, unaona wazi ni jinsi gani ukatili wa kijinsia unavyotesa wanawake. Mama huyu na mwanae wa kike wote wameangukia katika lindi la kufanyiwa ukatili.

MTANZANIA mwenzangu ni mara ngapi tumeshuhudia tukiwa safarini, wanaume wanavyowaomba madereva wasimame ili wajisaidie. Tena, kila wanapojisikia, wala hawajali kama ni mahali pa wazi au penye usiri.Tena wako baadhi ya madereva, wanaotumia fursa za wanaume kuwasimamisha  mara kwa mara, kuwapa pia  fursa hiyo abiria wengine, bila kujali kuwa sehemu husika haitawafaa wanawake. Huu ni UKATILI WA KIJINSIA.

Kisa mkasa cha pili, kadhalika. Ni wajibu wa madereva kuhakikisha kuwa sehemu wanazowapeleka abiria wao ‘kuchimba dawa’ zinakidhi mahitaji ya wanawake na wanaume kwa wakati mmoja?. Iwapo hazikidhi, basi watafute maeneo ambayo hayatakuwa ya  karaha hususan kwa wanawake na wasichana.

Jambo lingine kubwa na la msingi ni kwamba, mara nyingi wasafiri hawa huandamana na watu wanaowaheshimu. Ambao kwa mujibu wa tamaduni zetu, hawawezi wakaandamana nao ‘kuchimba dawa’ katika eneo moja. Lazima mmoja awe mbali na mwingine. Mfano, mama amesafiri na babake mzazi/baba mkwe. Au mtoto mwenye umri mkubwa amesafiri na mama yake mzazi/mama mkwe. Katika haya, WATANZANIA wenzangu tusidanganyane kwamba tunakwenda na wakati. Haya hayana wakati, tumezaliwa tumeyakuta na tutaendelea kuyaenzi kwa faida ya vizazi vijavyo.

 

Dominica Cassian Haule, ni Mwandishi wa Habari / Mchambuzi wa Masuala ya Jinsia   na Mwenyekiti wa Asasi ya Jinsia na Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania – GEMSAT.

dominicahaule@yahoo.com